Posts

UKURASA WA KITABU CHANGU

Image
Maisha yangu ni mfano wa kitabu kilicho na kurasa nyingi zisiso hesabika,zipo kurasa zinazo vutia-ambazo zingekufanya udondoshe mate baada tu ya kuzisoma,pia zilivo nyooka unaeza sema ni msitari ,aidha zipo ambazo zimekunjika na kuchafuka ila sikuonelea nizichane bali nilizitumia kama funzo mana kisicho kuua basi kitakukomaza. Yote kwa yote,ningependa kuwasilimulia mojawapo ya kurasa zangu ambazo zilichochea moto  na kupelekea mimi kujitosa  katika tasnia ya utangazaji Huenda mtu yeyote angenijuza miaka kumi iliyopita,kwamba ninge tumbukia Kwenye huba na uandishi au utangazaji kwa ujumla,nafkiri ningebisha a u  kudhani ni ndoto ambayo huenda ingebaki kuwa stori tu..Il a kwa uwezo wa Manani,safari hii ilipamba moto  baada ya kujiunga na Chuo Cha kiufundi Cha Mombasa ( TUM ),chuo ambacho nilitamani sana kujiendeleza kimasomo nilipokuwa shule ya upili,si kwa sababu ni miongoni mwa vyuo 20 bora hapa inchini,pia nimeshuhudia watu mashuhuri na wenye wadhfa waki...

ALMASI YA KESHO

Image
Kama safari ya kesho hupangwa Leo,kwanini kijana ambaye ni " kiongozi wa kesho" ashindwe kuandaliwa au kupewa uongozi katika muda huu.Licha ya haya yote, kijana ameendelea kudidimizwa na kunyimwa hata chembe ya fursa  ambayo angeweza kuonyesha uwezo wake.Wasicho kijua ni kwamba, vijana wakifua dafu na kukwea kimaisha, hata uchumi wetu utashamiri na kuitupa hali ngumu ya maisha katika kaburi la sahau . Picha kwa hisani ya iStock.com Ndiposa,ningependa kuwajuza jinsi vijana wanaweza kuleta uamsho katika uchumi wetu.Ila kabla sijawaeleza,ni vyema tukajiuliza je,hali au uwezo wa vijana wetu unaruhusu?Hapana.Hii ni kwa sababu asilimia kubwa wanaishi maisha ya kutikisa kiberiti ili waone kama ndani Kuna njiti, wengine wakivikumbatia vibarua ambavyo labda huwapa milo miwili kwa siku,kwa wale waliokosa unafuu basi hutaa taa  baada ya kukosa kabisa vibarua. Tumezungukwa na vijana wengi ambao wamekata tamaa maishani,ndoto zao wakizitupilia mbali na kukosa matumaini mithili ...

HALI SIO HALI!

Image
Kila mja angekuwa na uwezo wa kujichagulia maisha ayatakayo,basi hakuna ambaye angejitwika maisha yaliyo na fazaa au shida.Kila adinasi angejiweka mahali ambapo angefarijika zaidi.Mahali pasipo njaa,mafuriko,ukame,uwele au ugonjwa na mengineyo mengi yatakayo ikonga  nafsi yake,chambilecho wavyele kujiudhi haifai roho haina thamani. Je,ushawai jiuliza dhiki hizi huletwa na nini?Ngoja basi nikujuze,najua wapo ambao huenda wataviacha vinywa wazi, baada ya kujua kwamba, baadhi ya shida zinazotukaba hukaribishwa na hali ya hewa (ni athari hasi za hali ya hewa). Ila "hali ya hewa" au halihewa  imekua ikitafsiriwa kwa maana tofauti tofauti,wapo wanapolisikia basi fikra zao huchora mvua,jua au hata baridi shadidi, ingawa kitaaluma au kisayansi ni-namna ya kutaja yale yanayotokea katika sehemu ya chini ya angahewa, juu ya uso wa dunia katika eneo fulani na wakati fulani.(tafsiri hii ni kwa hisani ya Wikipedia). Hali ya hewa ikiwa nzuri,basi mambo hunyooka mithili ya mstari.Ila ikizidi...

TUMEPATA MWANGA BAADA YA KIZA KINENE

Image
Unapoizungumzia Mombasa,vitu sufufu hujijenga katika fikra yako,vitu kama;fuo za bahari,kivuko Cha feri bila kusahau pembe kubwa za alumini zilizojengwa kama kumbukumbu ya binti mfalme Margaret baada ya kuizuru Mombasa.Ndio! nazungumzia yale mapembe makubwa mawili yanayo patikana katika barabara ya Moi avenue. Ila fauka ya hayo,hivi unajua kipo kitu Cha thamani ambacho ni zaidi ya baraka kwa wakaazi wa Mombasa?hapa naizungumzia bandari ,kwani uchumi wa Mombasa na bandari ni kama shilingi kwa ya pili au tuseme vimevaana mithili ya Pete na kidole . Kwa miaka na mikaka,wakaazi wa Mombasa wamekua wakijivunia sana kwa uwepo wa bandari hiyo,hii ni kwa sababu ya ajira lukuki zinazo jitokeza na ukuzaji wa vipawa miongoni mwa vijana,kama unafikiri ni uongo basi muulize barobaro yeyote anaechezea timu ya Bandari f.c au ya mpira wa kikapu.Aha! tuna Kila sababu ya kuipenda bandari yetu. Ingawa zipo bandari zenginezo,kama ile ilioko;Lamu,Malindi,kiunga,kilifi,Mtwapa,shimoni,Funzi na Tan...

PENZI BOVU HALIFICHIKI

Image
Laiti kila mahuluki au mja angempenda mwenza wake kama anavyopendwa(anavyostahili),basi hakuna ambaye angeyachukia mapenzi.Hata nyuso za kila mwanandoa zingetawalwa na bashasha maana hawakukosea waliponena barua ya moyo husomwa juu ya panda la uso .Cha kusikitisha!  uhasama na kondo vimekua si jambo geni miongoni mwa walionaswa na kudidimizwa mapenzini,ila ushawai kujiuliza haya yote husababishwa na nini? Kwa mujibu wa ripoti zilizotolewa na baadhi ya mashirika hapa ulimwenguni: wanaojikuta wamo ndani ya mahusiano yaliyo na sumu ni wale walio na umri wa chini ya 35. Aidha hapa inchini kwetu mashirika kama:The standard,Nation pamoja na The star waliweka bayana jinsi vijana ususan walio katika vyuo vikuu,wanavyoteseka na mapenzi,ndiposa niliamua kulikazia macho swala hili.Hivyo basi Leo nitazungumzia kuhusu " penzi bovu au mahusiano yaliyo na sumu miongoni mwa wanavyuo". Vijana wengi huamini kuwa, muda sahihi wa wao kujitosa kwenye huba ni wanapoingia chuo kikuu,wen...

masaibu yanayo wakumba vijana katika jamii

Image
Ni changamoto sufufu zinazo wakumba vijana katika Karne hii,ila kabla hatuja zungumzia masaibu au changamoto hizo.Je,kijana ni nani?au anapaswa kuwa na miaka Kama mingapi? Maana au tafsiri zipo nyingi ila iliyo wazi na kujulikana na wengi ni-muda katika maisha ya adinasi/mtu kati ya utoto na utu uzima ususan miaka 15 hadi 29. Katika muda huu vijana hupitia masaibu lukuki,wengine huamua kukata tamaa ila wengine uamua kujiza titi na kupambana nazo.Ila leo tutazungumzia machache. Changamoto zenyewe ni kama zifwatazo 1.ukosefu wa ajira 2.dawa za kulevya 3.shinikizo la rika 4.wasiwasi wa muenekano wa kimaumbile 5.maswala ya kifamilia 6.uhalifu UKOSEFU WA AJIRA Swala hili limekua tatizi au tuseme kitendawili kisicho mteguzi miongoni mwa vijana wengi.Asilimia kubwa wamekua wakinyong'onyezwa na swala hili,wapo ambao walibahatika kusoma hadi chuo kikuu tena kwa kupata alama za kukonga roho za wengi,aidha wapo ambao hawakufua dafu masomoni hivyo basi kutokidhi matakwa ya muajiri,huenda.Fauka...