PENZI BOVU HALIFICHIKI

Laiti kila mahuluki au mja angempenda mwenza wake kama anavyopendwa(anavyostahili),basi hakuna ambaye angeyachukia mapenzi.Hata nyuso za kila mwanandoa zingetawalwa na bashasha maana hawakukosea waliponena barua ya moyo husomwa juu ya panda la uso.Cha kusikitisha! uhasama na kondo vimekua si jambo geni miongoni mwa walionaswa na kudidimizwa mapenzini,ila ushawai kujiuliza haya yote husababishwa na nini?
Kwa mujibu wa ripoti zilizotolewa na baadhi ya mashirika hapa ulimwenguni: wanaojikuta wamo ndani ya mahusiano yaliyo na sumu ni wale walio na umri wa chini ya 35.
Aidha hapa inchini kwetu mashirika kama:The standard,Nation pamoja na The star waliweka bayana jinsi vijana ususan walio katika vyuo vikuu,wanavyoteseka na mapenzi,ndiposa niliamua kulikazia macho swala hili.Hivyo basi Leo nitazungumzia kuhusu "penzi bovu au mahusiano yaliyo na sumu miongoni mwa wanavyuo".

Vijana wengi huamini kuwa, muda sahihi wa wao kujitosa kwenye huba ni wanapoingia chuo kikuu,wengine wakiamini ni wakati huu ndio wanaweza kumpata mwandani au mwenza wake wa maisha.Aidha wapo ambao huingia mapenzini kwa sababu ya uhuru wanaopata wakiwa chuo kikuu.Si vibaya!

Ingawa wapo ambao hubahatika na kumpata mpenzi ambaye huishia kufunga nae pingu za maisha,ila akali kubwa ni ya wale, wanaoamua kujitosa katika mahusiano kwa ajili ya maslahi yao binafsi.
Wapo wanaosema ukipata kigoli au kijana shababi katika chuo kikuu, hupaswi kuumpa mtima wako wote(au kujitosa mzima mzima kwenye mapenzi)ila huba linapo shamiri,huenda yote haya ukayasahau.Ikawa husikii wala huoni,huenda wavyele waliotuamba Haina tiba ndwele ya mapenzi pia hao yaliwakuta au walinaswa mapenzini.
Kabla sijasahau zipo sababu lukuki zinazo wafanya wanagenzi waingie au watake kuingia mahusianoni wakiwa vyuoni.Sababu hizo ni kama zifwatazo:

(I)HISIA-kama mnavyojua,binadamu tumeumbwa na hisia au kama wasemavyo tuna moyo sio jiwe,hivyo basi mida mengine moyo uhitaji barafu ya kuikosha.

(II)MAHITAJI YA PESA-wanaolengwa hapa sana sana,huwa ni vigoli ambao hutafuta mvulana ambaye kwao Kuna uwezo au anaye fanya kazi.Ndio! wapo vijana wanao soma na kujitaftia riziki,kwa hali kama hii kigoli hutumia mapenzi kama kisingizio Cha kujichumia fulusi,mwishowe yakawa mahusiano yanayo endeshwa kwa pochi.

(III)MAHITAJI  YA NGONO-wapo wanavyuo ambao hujikuta katika mahusiano kwa sababu ya ngono tu .Wala sio mapenzi ya dhati,kwa lugha inayo fahamika zaidi hit and run au one night stand.

(IV)USAIDIZI WA KIMASOMO-mwanagenzi humuadaa mwenzake,ili tu aweze kufaulu masomoni,hii ni kwa kumtumia ili amfanyie kazi zake.

(V)HAMU YA KUTAKA KUJARIBU-Shinikizo la rika huweza kuchangia pakubwa(mwanafunzi kutaka kujaribu mahusiano ili awe sawa na wengine).
Wengine kwa bahati mbaya kuangukia mahusiano yaliyo na sumu.

Sababu kama hizi na nyenginezo, humfanya mwanafunzi ajitose kwenye huba feki, wapo huishia kudhurika wengine kuishia kwenye mahusiano yenye vipigo,kero/dhiki/kinyaa au masimango 

na cha kusikitisha zaidi wengine huishia kujitanguliza kuzimu-kwa kujitia kitanzi au kunywa sumu au tuseme kwa kujitoa uhai.Hali kama hii,huzima ndoto za muathiriwa na si yeye tu,bali pia wazazi wake,ambao waliamua kuwekeza njenje/fulusi zao wakiwa na matarajio makubwa.Kwani wapo wazazi wanaouza urathi wote(kwa mfano mashamba) ili tu wamsomeshe mtoto wao,wapo wazazi wanaolala njaa ili tu mwana asome,wapo wazazi hutembea hatua nyingi ili tu mtoto wao apate nauli ya kufika chuoni.

Huenda tungefikiria haya yote,tungekua makini kabla kuingia mahusianoni au labda tusinge jaribu kuzichezea hisia za mwengine.

Na kama hayajakukuta usiseme siwezi fanya kitu fulani kwa ajili ya mapenzi,kwani heri kufa macho kuliko moyo.

Pia ningependa kuwajuza ya kwamba, mahusiano thabiti hujengwa kwa upendo wa kweli, ndiposa penzi bovu hujulikana tu unapo lipa muda,hivyo basi wanafunzi wawe makini, aidha wawekeze nguvu nyingi kutimiza ndoto zao.Ila ikitokea wavunjike moyo basi watumie hilo kama funzo kwani alokunyoa mekupunguza kuchana

WEWE NI WA THAMANI

Imeandikwa na kuchapishwa na;
SHEBAN JUMA
BANNIBOY THE PRESENTER 

Comments

  1. Mimi niwa thamani, mapenzi sumu subutu

    ReplyDelete
  2. Ni kweli sisi sote ni watu wa thamana ✨

    ReplyDelete
  3. Safi sana ❣️ MashaAllah Allah azidi kukupa Muongozo InshaAllah 🤲

    ReplyDelete
  4. Mimi ni WA thamai
    Inapaswa nijitunze
    Kazi safi

    ReplyDelete
  5. Mashallah Tabarakallah kazi nzuri mwanangu

    ReplyDelete
  6. Mawaidha na elimu muelekeo.
    Hongera kwa mwongozo mzuri.

    ReplyDelete
  7. Umewapa ushauri wa mana sana, Hongera kwa angalizo hili, sasa hiyari yao wakushika ashike anufaike, wakupuza kazi kwake. Nauthamini sana uwepo wako kwenye hili, mungu akutangulie kwa kila njema Inn sha Allah....

    ReplyDelete
  8. Hongera sanaa mwongozo mzuri
    na kazi nzuri ...Kipaji sana

    ReplyDelete
  9. Hongera sanaa mwongozo mzuri
    na kazi nzuri ...Kipaji sana

    ReplyDelete
  10. Hongera kazi nzuri 👍

    ReplyDelete
  11. Keep it up article nzuri sana

    ReplyDelete

Post a Comment

Popular posts from this blog

UKURASA WA KITABU CHANGU